Iraki
‘Nilidhani kupitia ndoa nitaweza kumaliza masomo’
Kalar, Iraq Akiwa na umri wa miaka 16 Shaikma aliolewa na mwanaume aliyekua kuwa mkubwa wake kwa miaka 12 ili kupunguza matatizo ya kifedha ya familia yake. Mara baada ya kuolewa, mume wake alimjeruhi kwa kumpiga na kumsababisha kupoteza jicho lake la kushoto kwa sababu aklikuwa anafanya mtalaa ya masomo ya sanaa katika chuo cha Sanaa mjini mwake. Shaima aliyedhani mumewe ana munga mkono ili kuendelea na masomo aliojaribu kujiua . Lakini alinusurika, na matokeo yake kuachwa na mumewe na kujikuta yuko pekee yake katika mji alikozaliwa katika jimbo la Kurdistan nchini Irak. Hii leo amerudi masomoni akisomea Sanaa, uigizaji na muziki.
Chapisho:
Baba yangu alikuwa askari wa Kikurdi wanaofahamika kama Peshmerga, na hali yetu ya kiuchumi haikuwa nzuri. Sisi ni watoto wanne nyumbani, wasichana watatu na mvulana mmoja.
Kwa hiyo nikaamua kubeba baadhi ya majukumu. Sikutaka kuwa mzigo kwao lakini sikuweza kupata kazi ya aina yeyote.
Ilikuwa ngumu sana kupata kazi. Kwa hiyo ilibidi niolewe kwasababu nilifikiri kwa kupitia ndoa ndio nitafanikiwa kumaliza shule.
Nilifikiri mume wangu ataniunga mkono lakini kwa bahati mbaya, hakufanya hivyo, badala yake alinitesa.
Akiwa ameolewa mwaka 2014 akiwa na umri wa miaka 15, Shaima bado anambeba doli wake wa utotoni Baada ya kuachwa katika hali mbaya ya ndoa. Shaima anasema rafiki zake wanamdharau.)
Nilipata leseni yangu ya kuolewa katika mahakama ya Kalar, wilaya ya Khanaqin, ambako wasichana walio na umri mdogo wanapata ruhusa ya kuolewa kirahisi.
Katika umri mdogo sana unachukua majukumu mazito, yanakuzidi kwasababu hujui nini cha kufanya katika umri huo au ukiwa kama mama au mke.
Kwa kawaida unahitaji muda wa kudekezwa lakini unapoolewa na kuwa na watoto inakubidi kuwahudumia wengine.
Maisha yalikua magumu sana baada ya kuachwa. Nilikumbwa na hali ngumu. Nilipata msongo wa mawazo kwa sababu sikuweza kuishi maisha ya kawaida. Nilikua na uoga na machofu. Nilikuwa na wasi wasi jinsi gani watu wanavyonifikiria .
Katika jamii hii, ya watu wasiofikiria mambo nje ya jamii yao, watu wanadharau wanawake walioachwa.
“Ili kupunguza machungu yaliyonipata, nilijihusisha katika michezo ya kuigiza, ili kusahau mateso, nikajiwezesha na kupata maarifa zaidi.” To alleviate my suffering, I got involved in theater, acting, to forget my pain, become empowered, and enhance my skills.”
Kabla ya kuolewa Shaima alikuwa na ndoto za kwenda chuo kikuu. Sasa baada ya kurudi nyumbani anafundisha michezo ya kuigiza, sanaa na muziki. Anataka kuondoka Iraq. Amesema yuko kuolewa kwa mara ya pili ili watu waache kumsema.
Ili kupunguza machungu yangu, nimejihusisha na michezo ya kuigiza, ili kusahau mateso yangu na kupata uwezo na kuongeza ujuzi wangu.
Nimeshiriki katika tamasha mbali mbali za kimataifa na nilipata zawadi ya muigizaji bora wa pili.
Miezi miwili baadaye mjini Baghdad nilicheza katika filamu ya ‘Shaqam.’ Mataifa mengine kadhaa yalishiriki ikiwa ni pamoja na Iran, Misri, Qartar, Tunisia na miji mingi ya Iraq.
Mchezo wetu ulikuwa kuhusu janga la Shingal na wasichana wa Yazidi. Niliandika mchezo huo kwa msaada wa Bw.Hunar mwalimu mjini Koya. Kila mmoja alipenda mchezo wetu na kupata tuzo ya mwigizaji bora wa kike.
Nawaomba wazazi: Msiruhusu watoto wenu kuolewa wakiwa chini ya umri wa miaka 18. Msiwaache wafanya maamuzi yao wenyewe, kwasababu wakati wa umri huo hawajapevuka, hawawezi kufanya maamuzi bora juu ya siku zao zijazo.
Mpaka pale watakapofika umri wa miaka 18 ndio wazazi watoe ruhusa kwao kuamua kuhusu wakati gani wanataka kuolewa.
Mtizamo wa Kimataifa
10% | 20% | 30% | 40% | 50% | 60% |