Jinsi Ebola ilivyodhibitiwa DRC

Mlipuko wa Ebola nchini Kongo umefuatiliwa kwa karibu na , mpaka sasa, umedhibitiwa ipasavyo, ukilinganisha na mlipuko kama huo uliotokea Afrika Magharibi 20`14, na kuuwa maelfu ya watu.

Mlipuko huo wa Ebola huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo unaonekana kuwa umefikia ukingoni. Licha ya kuwepo vifo 28 mwanzoni mwa mwezi Juni , viongozi wa afya kwa uangalifu wana matumaini kuwa wameanza kuudhibiti mlipuko huu. Hadi sasa, ni mageuzi ya kustaajabisha kulingana na mlipuka wa Afrika Magharibi 2014, ambao uliuwa watu zaidi ya 11,000 huko Liberia, Sierra Leone na Guinea, na maambukizi hayo yalifika hadi Glasgow, Scotland, na Dallas, Texas.

Licha ya ugumu wa kutembea kufika maeneo yasiyokuwa na barabara na jamii kuwa wana mashaka na wahudumu wa afya, mwanzoni kabisa wa mlipuko huu, maafisa wa afya walikabiliana na maradhi hayo na kuweza kuyadhibiti. Sababu kadhaa zilifanya hatua zilizochukuliwa DRC kuonekana kuwa tofauti, kuliko zile zilizo chukuliwa wakati wa milipuko ya nyuma, na kuweza kuokoa maisha ya watu wengi.


1. Umbali kati ya vijiji mbalimbali na miundombinu iliyokuwa duni ilichelewesha kuenea kwa maradhi hayo.

Kutokana na masafa ya kufikia maeneo mbalimbali nchini DRC iliwia vigumu kwa watoa huduma ya afya kufikia jamii zilizokuwa zimeathirika, lakini pia ilizuia kuenea kwa maradhi hayo. Katika maeneo mengi , watu waliokuwa wameathirika walibakia katika jamii zao, na watu wa nje hawakuweza kufika katika maeneo yaliyo athirika, hivyo kupunguza sana idadi ya maambukizo. Lakini ikilinganishwa na mwaka 20`14, wakati wa kilele cha maambukizo huko Afrika Magharibi, Ebola ilienea kwa haraka katika miji iliyokuwa ina idadi kubwa ya watu.

“Sio kwamba hakuna kabisa hatari ya maambukizo. Hilo sote tunatakiwa tulizingatie. Vihatarishi vya virusi kuweza kupenya katika nchi nyingine bado vipo. Lakini kwa hatua zilizochukuliwa - hatua madhubuti zinazochukuliwa na serikali hivi sasa -inaweza kupunguza kuenea kwa maambukizi ya maradhi haya, kwanza nchini Kongo, na kisha katika nchi za jirani.”

Picha ya Djoudalbay Benjamin

Djoudalbaye Benyamini Mkuu wa Sera na Diplomasia ya Afya, Vituo vya Afrika vya Kudhibiti na Kuzuia Maambukizi ya Magonjwa

A 'Play' button icon
Ramani ya DRC
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ni nchi ya pili kwa ukubwa Afrika kwa eneo la ardhi, na ya nne kwa wingi wa watu. Imekuwa pia inakabiliwa na kuzuka kwa Ebola zaidi kuliko nchi nyingine yoyote. Kuongezeka kwa mlipuko 2018, ambao ni mlipuko mkubwa wa saba katika historia ya DRC kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani. Kirusi kiligunduliwa huko mwaka 1976. (VOA)

2. Chanjo yenye ufanisi mkubwa, iliyokuwa ikiendelezwa kwa zaidi ya muongo mmoja lakini haikutumika hadi mwisho wa mlipuko uliotokea Afrika Magharibi, na ilitumika bila ya kuchelewa huko DRC.

Chanjo, V920, ingawa bado iko kwenye majaribio, imeonyesha kuwa yenye ufanisi mkubwa katika kuzuia maambukizi ya Ebola . Ni vigumu kuisafirisha na inapatikana kwa uchache sana. Lakini maafisa wa huduma za afya wamepata njia ya kutatua tatizo hili.

“"Chanjo ni virusi vyenye uhai. Ina kirusi kidogo cha Ebola lakini protini inayokifunika kirusi hicho cha Ebola, haina madhara. Na hivyo basi kinajitengeneza kwa wingi ndani ya mwili na kuufanya mwili uweze kutengeneza kinga yake - mfano kama ule wa seli zenye kutengeneza kinga ambazo tunaamini zinaulinda mwili."”

Picha ya Beth-Ann Coller

Beth-Ann Coller Mkurugenzi Mkuu, Kiongozi wa Mradi na Usimamizi, Merck na Co.

A 'Play' button icon

Madawa hayo husafirishwa katika makontena maalum ambayo yanahifadhi joto chini ya kiwango kinacho hitajika cha digrii 60. Na wanatoa chanjo hiyo kwa kutumia utaratibu wa "chanjo ya mduwara" ambayo inahusisha kuwafikia watu ambao wana uwezekano mkubwa wa kugusana na wagonjwa wenye mambukizi.

Picha ya mfanyakazi wa WHO
Katika picha hii iliyochukuliwa Alhamisi, Mei 31, 2018, mfanyakazi mmoja wa Shirika la Afya Duniani anashikilia chanjo ya Ebola huko Mbandaka, Kongo. Kwa mara ya kwanza tangu kirusi cha Ebola kilipo gundulika zaidi ya miaka 40 iliyopita, chanjo imepelekwa kwa wafanyakazi wa afya walio mstari wa mbele katika juhudi zao za kupambana na janga hilo la Ebola mara tu lilipoanza . (AP Photo / Sam Mednick)

3. Wananchi wa maeneo hayo wamepokea kwa moyo mkunjufu hatua iliyo chukuliwa na wahudumu wa afya.

Wakazi wamehoji nia ya wafanyakazi wa huduma za afya, ufanisi wa chanjo ya majaribio na iwapo kama Ebola ni ugonjwa wa kweli. Licha ya kuwa na wasiwasi huu, jamii zilizoathiriwa zimeendelea kukubali kupatiwa chanjo.

“Kama ukiweza kufikiria, kuwa kuwepo kwa virusi vya Ebola katika jamii ni jambo la kutia wasiwasi kwa wakazi wa eneo hilo. Na ndiyo sababu ilikuwa muhimu, kwa kweli, kuwa na timu za wahamasishaji wa kijamii na wataalam wa jamii ambao wanatumika kuhakikisha kuwa kila kitu kinafafanuliwa na kuwekwa wazi kwa jamii hizo.”

Picha ya Tarik Jaservic

Tarik Jasarevic Msemaji wa Shirika la Afya Duniani

A 'Play' button icon

Kuanzia Juni 10, watu 2,295 wamepatiwa chanjo katika maeneo ya Wangata, Iboko na Bikoro. Wale walio chanjwa kati yao ni wafanyakazi wa afya walio mstari wa mbele katika kukabiliana na Ebola, na watu waliogusana na wagonjwa ambao wamethibitishwa kuwa na Ebola, na wale walio kuwa wanakutana nao.

Viongozi wamefanya kampeni mbalimbali za uhamasishaji, ikiwa ni pamoja na kutumia vyombo vya habari, kutoa mafunzo kwa waandishi wa habari wa maeneo hayo na kufanya mikutano na viongozi wa mitaa, WHO imesema.

Picha ya familia nchini DRC.
Katika picha hii iliyochukuliwa Ijumaa, Juni 1, 2018, familia imeketi nje katika eneo jirani ambako watu watatu walikufa kutokana na Ebola mwezi uliopita, huko Mbandaka, Kongo. Kwa mara ya kwanza tangu virusi vya Ebola kugundulika zaidi ya miaka 40 iliyopita, chanjo imetumwa kwa wafanyakazi wa afya walio mstari wa mbele kupambana na janga hilo la Ebola mara tu lilipozuka. (AP Photo / Sam Mednick)

4. Miundombinu ya kimataifa illiyoboreshwa kuweza kukabiliana na milipuko wa ugonjwa huo imethibitisha kuwa na ufanisi.

Wakati Ebola ilipo ikumba Afrika Magharibi tangia mwishoni mwa 2013 hadi mwanzo wa 2016, bara hilo halikuwa na taasisi kuu ya kusaidia kuzuia, kufuatilia na kusimamia hatua za dharura za kukabiliana na magonjwa ambukizi. Lakini hilo lilibadilika mwezi Januari 2017, kwa kuzinduliwa Vituo vya Udhibiti wa Magonjwa Afrika.

“Tuna uwezo wa kujua hatari za afya ya umma kwa haraka zaidi na kisha kukabiliana nazo mara moja bila ya kuchelewa na kwa juhudi zote. Na hayo ndiyo mabadiliko makubwa tulio yashuhudia wakati huu. Tumepeleka, kama nilivyo sema, watu zaidi ya 150 ndani ya siku 10 baada ya kuthibitishwa mlipuko huu. Na tumeungwa mkono kwa nguvu zote na washirika wetu. Iwe ni shirika la madakatari wasio na mpaka, Médecins Sans Frontières, Shirika la Mpango wa Chakula Dunia, Shirika la UNICEF au Shirika la Msalaba Mwekundu na Shirika la Red Crescent, tumekuwa na msaada mkubwa kutoka kwa washirika ili kuhakikisha kila kitu kinafanya kazi vizuri kabisa katika kukabiliana na suala hili la Ebola.”

Picha ya Peter Salama

Peter Salama Shirika la Afya Duniani Dunibu Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Kuandaa na Dharura ya Dharura

A 'Play' button icon

Kama sehemu ya Umoja wa Afrika, CDC ya Afrika inalenga kuboresha miundombinu ya afya ya bara hili. Katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ambayo imehusisha kusaidia jitihada za kitaifa kupitia kituo cha operesheni ya dharura, kupeleka timu ya kukabiliana na janga la mlipuka huo na kutenga $ 250,000 kusaidia kukabiliana na mlipuko huu.


5. Ramani, picha za satelaiti na vyanzo vingine vya takwimu vilivyo kuwa na taarifa ya kufanya maamuzi mara moja yenye ufahamu sahihi.

Umbali wa maeneo ya Kongo na miundombinu duni ilitoa changamoto kwa wafanyakazi wa huduma za afya kuweza kuwafikia waathirika wa Ebola. Taarifa za takwimu za idadi ya watu zilizopitwa na wakati na ramani zilizokuwa sio sahihi zilisabibisha ugumu zaidi kutoa huduma kwa sababu maafisa wanategemea takwimu sahihi ili kuweza kufahamu mlipuko utadumu kwa muda gani.

Ramani ya DRC inayoonyesha eneo lililoathirika na mlipuko wa Ebola 2018.
Ramani ya DRC inayoonyesha picha iliyokuzwa ya eneo hilo lililoathiriwa na mlipuko wa Ebola 2018.
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ni nchi ya pili ya Afrika kwa ukubwa kwa eneo la ardhi. Mlipuko wa 2018 uliathiri mikoa mitatu katika sehemu iliyoko masafa ya mbali magharibi ya nchi hiyo, karibu na mpaka wa Jamhuri ya Kongo.

Hilo ilisababisha wataalam kama Koreshi Sinai, mchoraji wa ramani ya UCLA, kushiriki.

Sinai alifanya kazi na Wizara ya Afya, The Atlantic iliripoti , kujadidisha ramani za zamani, zisizo sahihi na kufanya "sensa ndogo" ili kukadiria idadi mbalimbali za watu.

Mipango pia inaendelea kujenga database ya bara zima. Hiyo itasaidia katika kupata taarifa zitakazo saidia juhudi za kukabiliana na mlipuko siku za usoni.

Mikopo

Dan Joseph alihariri hadithi hii.

Jackson Mvunganyi na Paul Alexander waliripoti kwa Afrika News Tonight.

Greta Van Susteren waliripotiwa kwa Kuunganishwa na Greta Van Susteren.